Rose Ndauka Atoa Siri ya Mambo Yake Kumnyookea

Thursday, 19 May 20160 comments


 MKALI wa filamu Bongo, Rose Ndauka ametoa siri ya mambo yake kumnyookea kuwa imetokana na kumuhusisha Mungu kwa kila anachokifanya na wala si vinginevyo kama watu wanavyodhania.

Akizungumza na Amani, Rose ambaye kwa sasa anamiliki kampuni inayojishughulisha na kutengeneza Jarida la Rozzie, alisema kuwa Mungu ndiye aliyemtendea miujiza hiyo kwani asingemshirikisha asingekuwa hapo alipo.

“Siri kubwa ya mafanikio niliyonayo ni kumtegemea Mungu na hakuna namna yoyote kinyume na hapo niliyofanya. Kuna faida kubwa sana katika maisha yangu, nimeona na nimeshuhudia kabisa, wala sitathubutu kumuacha kamwe,” alisema Rose.
Share:  
Weka Maoni yako Hapa
Share this article :
TOA MAONI HAPA

Post a Comment

 
Copyright © 2011. brotherlucastv - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger